FIND UR TRUE LOVE

Saturday, January 7, 2012


 
 
Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Dar es Salaam  kimemtaka  Waziri wa Ujenzi John Magufuli aache kufanya kazi kwa jazba, dharau na maneno ya kejeli.

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita, alisema jana kuwa hawakufurahishwa na lugha ya kibabe aliyotoa Magufuli alipozungumzia sakata la kupanda kwa nauli za kivuko cha Kigamboni.

Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Guninita alisema kuwa kauli aliyoitoa Magufuli kwa mbunge wa Kigamboni Faustine Ndungulile na wananchi ya kuwataka kupiga mbizi na kwamba mbunge wa Kigamboni kama anawaonea huruma wananchi anunue boti itakayoitwa kwa jina lake au chama chake ni kauli inayotia hofu na inaweza kupoteza wanachama, na chama hicho kimkoa kimemtaka awaombe radhi wananchi kutokana na kauli yake hiyo, “Kuna haja viongozi wachague kauli ya kusema na sheria zimetungwa na kutengenezwa na watu na zinazungumzika, ukifananisha vivuko vya Ziwa Victoria na hiki cha Kigamboni ni tofauti kubwa na neno ‘marufuku’ si neno jema hivyo ni busara kuomba radhi,” alisema Guninita.

Guninita alisema kauli hiyo ya Magufuli haijengi mshikamno na ushirikiano kati ya viongozi wa CCM, serikali ya mkoa na wananchi, na kwamba kama malalamiko ya wananchi hao hawezi kuyasikiliza, asingetumia maneno aliyoyasema.

Aidha Guninita alisema kuwa CCM mkoa wa Dar es Salaam, imeipokea kwa masikitiko kauli hiyo na imewaomba wananchi kuwa na subira wakati uongozi wa chama ukiendelea na jitihada za kuzungumza na serikali ili kutatua tatizo hilo kwani umesikia kilio chao cha kupanda kwa nauli na unawathibitishia kutatua tatizo hilo.

 
 
 
Muasisi na Mwenyekiti wa kwanza wa Chama cha Wananchi (CUF), James Mapalala, amesema yanayotokea ndani ya chama hicho hayamshangazi kwa kuwa Katibu Mkuu Maalim Seif Sharif Hamad alitumia watu ‘walevi’ kumfukuza ndani ya chama hicho mwaka 1994.

Akizungumza kwa njia ya simu na Tanzania Daima, Mapalala alisema Maalim Seif ni kiongozi anayewatumia baadhi ya wanachama wake kupata mafanikio, na kisha hutumia nguvu kuwafukuzwa kwa vitimbi kama alivyofanyiwa yeye na sasa Hamad Rashid Mohamed.

Alidai kuwa Maalim Seif aliwahi kumtumia yeye kama daraja mwaka 1992 kwa kuzunguka nchi nzima bara na Zanzibar, akilala vijijini kwa lengo la kukitangaza chama ili waweze kuwakomboa wananchi wanyonge lakini matokeo yake alimfukuza kwa visingizio mbalimbali ambavyo si vya kweli.

Mapalala alienda mbali zaidi na kueleza kuwa Maalim Seif si mtu wa kawaida hasa unapogusia masuala ya madaraka kwa kuwa ni mtu ambaye anapenda fedha na madaraka, huku akiyatumia vibaya kwa kuwakandamiza wanyonge, “Hakuna mtu ndani ya CUF asiyejua kwamba Hamad Rashid alikuwa ni mtu muhimu sana ndani ya chama hicho kwani ndiye kiongozi wa pekee mwenye uwezo wa kutafuta fedha nje ya nchi kwa ajili ya kuendesha chama, lakini Maalim amemtimua kama ilivyokuwa kwangu baada ya kufanikiwa kupata mafanikio mbalimbali hadi kuwa Makamu wa Rais,” alisema Mapalala.

Mapalala alidai kuwa Maalim Seif anapenda kila atakalosema yeye ndilo litendwe na watu wote ndani ya chama bila kuzingatia maoni ya watu wengine hata kama si jambo zuri kwa maslahi ya chama.

Akizungumzia kufukuzwa kwake ndani ya chama, alisema kuwa mwaka 1994 katika mkutano uliyofanyika mkoani Tanga alitimuliwa bila kupewa sababu za msingi na kwamba waliofanya maamuzi katika mkutano huo hawakuwa wanachama halali na nakala za barua na majina yao anayo hadi sasa.

Aidha aliwaonya viongozi mbalimbali wa CUF kuwa wanapozungumzia matatizo yao ndani ya chama hasa katika kipindi hiki ambacho wamemfukuza Hamad wasitolee mfano jina lake kwa kuwa ana vielelezo vyote vya Maalim Seif na wenzake kutumia ‘walevi’ wa pombe ambao walihongwa huku wakiwa si wajumbe ili waweze kunifukuza, “Tena sitaki kabisa wasijipe umaarufu kusafisha dhambi zao kwa kunitaja mimi. Katika mkutano ule wa Tanga waliokuwa wameitisha kwa ajili ya kunifukuza mimi, nilipewa barua masaa machache na kwamba mkutano ulifanyika usiku, wajumbe walikuwa si halali na vielelezo hadi sasa ninavyo wasitake niwaumbue,” alisema Mapalala.

Mapalala alisema Maalim Seif bila kujiingiza katika migogoro alitakiwa kuangalia hali ya wananchi wa Zanzibar hasa Pemba ambao tangu kuingia kwa serikali ya mseto mambo ndiyo yamezidi kuwa magumu zaidi, “Sharif Hamad ni kiongozi ndani ya CCM ndio maana anashindwa kuwatetea wananchi, ameua chama; watu wanahoji anakuja juu, watu wanahoji matumizi ya fedha anakuja juu, ni mtu ambaye anapenda sana madaraka na hili ndilo tatizo kubwa ambalo linaua demokrasia ndani ya vyama hasahasa chama hicho,” alisema Mapalala.

Aidha alimshauri mbunge huyo wa Wawi kama ana nia ya kuwakomboa wananchi hasa wakazi wa Pemba basi aendelee kwa kuanzisha chama chake asirudi CCM kwa kuwa chama hicho ndicho kimeungana na Maalim Seif.

Mapalala ambaye ni mwenyekiti wa chama cha Chausta amemkaribisha Hamad Rashid kujiunga nacho kwa vile anaamini ni kiongozi makini na mchapa kazi hodari.
---
via  Tanzania Daima
 
 
Picture
photo by "Bellringersly" via flickr
Huko Dodoma, madaktari wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma wameendelea na msimamo wa kutofanya kazi hadi watakapolipwa fedha zao huku utoaji wa huduma kwa wagonjwa ukiendelea kudorora.

Mgomo huo wa madaktari ambao ulianza juzi asubuhi umesababisha wagonjwa wengi waliolazwa na wale wanaofika hospitalini hapo kukosa huduma zinazostahili.

Madaktari hao wamegoma wakishinikiza Wizara ya Afya iwalipe fedha zao za miezi miwili wanazodai.

Zaidi ya madaktari 33 wanaidai wizara hiyo malipo ya fedha kuanzia mwezi Novemba na Desemba mwaka jana ambazo hawajalipwa hadi leo.

Hata hivyo, kaimu mganga mkuu wa hospitali ya mkoa, Dkt. Nassoro Mzee, alisema malipo ya madaktari hao yanashughulikiwa baada ya fedha kufikishwa Hazina ndogo ya Dodoma, “Fedha zimeshafika na zipo kwenye utaratibu wa malipo, naamini hadi Jumatatu madaktari wote watakuwa wamelipwa fedha zao,” alisema.

Hata hivyo, katibu wa hospitali hiyo, Isaack Kaneno, alisema madaktari hao wamekataa kuingia kazini hadi wapate fedha mkononi, licha ya kuambiwa kuwa ziko Hazina na zinashughulikiwa, “Inasikitisha kwamba wenyewe wanadai mwezi mmoja na hapohapo kuna watumishi wengine wa serikali wanadai miezi mingi, mbona hawajagoma?” alisema.

Hata hivyo, katibu mkuu alisema kwa mujibu wa taratibbu za kazi, mfanyakazi akigoma kwa siku tatu mfululizo atakuwa amejifuta kazi mwenyewe.

- via Tanzania Daima
 
 
Picture
photo by "MADAKTARI" via flickr
Uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) umewapa barua za kurudi Wizara ya Afya madaktari 229 walioko katika mafunzo kwa njia ya vitendo kutokana na mgomo wa siku nne wakishinikiza kulipwa posho zao za mwezi mmoja.

Hatua ya kuwafukuza madaktari hao kwa barua hizo, imesababisha huduma za afya kudorora na kuna madai kwamba baadhi ya wagonjwa walikosa huduma kwa siku nzima ya jana kutokana na kutokuwepo kwa madaktari.

Mkurugenzi wa hospitali hiyo, Dkt. Marina Njelekela, tangu juzi alikataa kuzungumza na waandishi wa habari, na kutwa nzima ya jana simu yake ya kiganjani ilikuwa ikiita bila kupokelewa.

Madaktari hao walifukuzwa kupitia tangazo la barua iliyosainiwa na Dkt. Marina Njelekela kisha kubandikwa katika kila wodi za hospitali hiyo likibeba kichwa cha habari: ‘Kuhusu kurudishwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii’.

Kwa mujibu wa tangazo, uongozi wa Muhimbili umewataka madaktari hao kuchukua barua zao ili waende Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kupangiwa kazi katika vituo vingine, kwa vile hawatakiwi tena pia.

“Mara upatapo barua hii unatakiwa kujeresha vifaa vyote ulivyopewa na hospitali vikiwemo funguo za chumba na kitambulisho na kuripoti Wizara ya afya mara moja,” ilisema sehemu ya barua hiyo ambayo nakala yake pia imepelekwa kwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi Jamii, Blandina Nyoni.

Kwa mujibu wa barua hiyo madaktari hao wamekiuka makubaliano ya kifungu namba 1(b)(d) (e) (f) (g) kama ilivyoelekezwa na Katibu Mkuu katika barua yake ya kuwapangia mafunzo katika Hospitali ya Muhimbili.

Habari kutoka ndani ya hospitali hiyo zinaeleza kwamba madaktari hao walirejea kazini jana majira ya saa 11.00 alfajiri wakiwa wamevalia nguo zao za kazi na kabla hawajaingia wodini walizuiwa na walinzi wakitakiwa kuangalia matangazo yaliyoeleza kusimamishwa kwao kazi.

Akizungumza na waandishi wa habari hospitalini hapo kiongozi wa madaktari hao wanafunzi, Dkt. Deogratias Mally, alisema wanashangazwa na hatua ya uongozi kuwasimamisha kazi wakati mkataba wao unatambuliwa na Wizara ya Afya.

Alisema wakati wanadai haki yao hawakuitisha mgomo, hivyo wanashangazwa na hatua ya uongozi huo kuingilia suala ambalo lilitakiwa kufanywa na wizara kwani hata mkataba wao wa ajira hausemi hivyo, “Barua ya madai yetu tuliandika kwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya na si Mkurugenzi wa Muhimbili,” alisema Dk. Mally.

Alisema kutokana na hali hiyo jana walijipanga kumtafuta mwanasheria na kukaa naye ili watafakari walipokosea ili baada ya kikao na mwanasheria huyo Jumatatu ijayo waende wizarani.

Mgomo huo wa madaktari ulianza mwanzoni mwa wiki hii kwa madaktari hao kushinikiza kulipwa jumla ya sh milioni 176 ambazo ni posho zao za kujikimu za mwezi Desemba mwaka jana. Kwa maelezo yao walidai hawatamaliza mgomo huo hadi hapo watakapolipwa fedha hizo. Hata hivyo juzi jioni walianza kulipwa baada ya serikali kusalimu amri.


via Tanzania Daima

mafuroko tanzania yamekuwa sio ya kawaida ,sasa wanaichi wanapata tabu mpaka chakula maji umeme shida tanzania je?watanzania wankuwa hawana haki ,ndani ya inchi hii viongozi wanajinufaisha maisha yao kuwa mazuri leo ,leo viongozi wana kuwa hawana habari ya walio wachagua jamani fungueni macho wana inchi amkeni katiba zinabadilishwa kwa ajili ya maslahi ya vigogo

Wednesday, September 28, 2011

Helikopta ya Chadema yatikisa Igunga

MBILI ZA CCM ZASHINDWA KUTUA ZABAKI KIA, YA  CUF KUPASUA ANGA LEO 
Waandishi Wetu, Igunga
WAKATI Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jana kilitikisa anga la Igunga baada ya kuanza kutumia helikopta kufanya kampeni zake, zile mbili za wapinzani wao, CCM zikishindwa kuwasili jimboni humo na kubaki Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kutokana na sababu za kiufundi.Wakati Chadema ikipasua anga na mbili za CCM zikibaki KIA, helikopta ya Chama cha Wananchi (CUF) nayo imeshindwa kutua Igunga jana na sasa inatarajiwa hapa leo.

Helikopta ya Chadema ilianza kuonekana katika anga la Igunga saa 10:40 jioni ikiwa na maandishi makubwa ya chama hicho na rangi ya bluu.Ujio wa helikopta hiyo ulivuta kwa muda idadi kubwa ya wananchi waliokuwa kwenye Viwanja vya Sabasaba wakisubiri ujio wa helikopta mbili za CCM, ambazo awali

ilielezwa kuwa zingewasili saa 8:00 mchana.

Baadaye ilielezwa kwamba helikopta hizo za CCM zingetua Igunga saa 11:30 jioni zikiwa na makada wa chama hicho akiwamo Katibu wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Bumbuli, January Makamba.

Hata hivyo, ilipofika saa 12:00 jioni, Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde akitumia gari la matangazo la Bendi ya muziki ya ToT Plus alitangaza kwamba helikopta hizo zisingeweza kutua Igunga kutokana na sababu za kiufundi.
Alisema zilichelewa kupata vibali kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Dar es Salaam na kwamba baada ya kutua KIA ilishauriwa kuwa ni vyema zilale hapo.

Alisema kama helikopta hizo zingeondoka KIA jana jioni na kufika hapa usiku wakati tayari kungekuwa na giza kitu ambacho kisingekuwa kizuri kiusalama. Alisema helikopta hizo sasa zitawasili leo saa 4:00 asubuhi.

Matumizi hayo ya helikopta yanawafanya wananchi wa Igunga kushuhudia kampeni nzito na za aina yake tangu kufanyika kwa uchaguzi wa kwanza wa vyama hivyo mwaka 1994 na Rostam Aziz kushinda.Jimbo hilo lenye wapiga kura 170,000 katika vijiji 96, halijawahi kushuhudia kampeni nzito kiasi hicho zinazohanikizwa na magari yenye vifaa vya kisasa vya muziki.

Habari kutoka ndani ya CCM, zinaeleza kuwa katika kujihakikishia kura katika kipindi hiki cha lala salama, chama hicho kitawatumia makada wake, Makamba na Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli wanaoelezwa kuwa na ushawishi mkubwa.

Kulingana na vyanzo mbalimbali vya habari, Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa aliyekuwa mgeni rasmi katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni za CCM anatarajiwa kurudi tena hapa keshokutwa.Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe naye aliwasili hapa jana kuongeza nguvu kwa viongozi wa chama hicho ambacho idadi kubwa ya wabunge wake wameweka kambi hapa.

Helikopta ya CUF
Kwa upande wake, CUF kinatarajiwa kuanza kutumia helikopta yake kuanzia leo huku Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Juma Duni Haji akitarajiwa kufunga pazia la kampeni za chama hicho ambazo, awali zilitarajiwa kufungwa na Katibu Mkuu wake ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharrif Hamad.

Akizungumzia na waandishi wa habari jana, Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Bara), Julius Mtatiro alisema kampeni hizo sasa zitafungwa na Haji anayetarajia kuwasili wakati wowote katika kipindi hiki cha mwisho wa kampeni.Mtatiro alisema tayari wabunge wa chama hicho  akiwamo Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Zanzibar) Ismail Jussa wanaendelea na kampeni jimboni humo.

CCM, Chadema vyatuhumiana
Kiwewe cha uchaguzi huo kimezidi kutesa vyama vya CCM na Chadema, baada ya kuendelea kutuhumiana huku chama tawala kikidai kunasa kile ilichokiita mpango wa siri wa wapinzani wake hao wa kujitangazia ushindi kabla Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kufanya hivyo.

Chadema nacho kimekituhumu CCM kwamba kimeandaa mpango wa kupeleka wapigakura mamluki kutoka katika baadhi ya mikoa ukiwamo Dar es Salaam.

Jana, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Steven Wassira aliwaambia waandishi wa habari mjini hapa kwamba Chadema kimepanga mpango huo wenye lengo la kuwaandaa wanachama wake waone wameibiwa kura pindi CCM kitakapotangazwa mshindi.“Tunazo taarifa za uhakika kuwa wamepanga kutumia magari ya matangazo kutangaza kuwa Chadema imeshinda, hata kabla ya kura kuhesabiwa ili wapate leseni ya kuanzisha vurugu,” alisema Wassira.

Wassira ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uhusiano), alisema tayari CCM wameviarifu vyombo vya ulinzi na usalama ili kuchukua hatua na pia kuwaelimisha na kuwasihi wananchi kutoingia katika mtego huo.

“Lengo ni kuwaharibu vijana kisaikolojia kwamba yakitangazwa matokeo tofauti waone wamechakachuliwa kura zao na CCM. Tunawasihi Chadema na wanachama wao watulie wakati wananyolewa,” alisema Wassira.

Wassira alisema wanakusudia kutumia mikutano ya hadhara ya kampeni iliyobakia wiki hii ya lala salama, kuwaeleza wananchi juu ya mpango huo wa Chadema ambao alidai hauwatakii mema wananchi wa Igunga.

Hata hivyo, Mratibu wa Kampeni za Chadema  Igunga, Mwita Waitara alikanusha vikali madai hayo akisema hawana sababu ya kufanya hivyo kwa kuwa wananchi wameshafanya uamuzi wa kuikataa CCM.“Wassira anafahamu utaratibu wa kutangaza matokeo ulivyo kwamba Chadema hatuna uwezo huo. Hivi kama tulikuwa na uwezo huo kulikuwa na sababu gani ya kufanya kampeni na kuteua hadi mawakala?,” alihoji.

Alikishutumu CCM akidai kuwa kina mpango wa kuingiza watu 1,050 kutoka Mikoa ya Dar es Salaam, Singida na Shinyanga ili watumie shahada bandia kukipigia kura chama hicho tawala.Waitara alidai kuwa watu 500 watatoka Dar es Salaam, 300 Singida na 250 Shinyanga lakini akasisitiza kuwa Chadema kina mtandao mpana na kitahakikisha kinazuia mpango huo usifanikiwe.

Chagonja atua Igunga

Kamishina wa Polisi anayeshughulikia Operesheni na Mafunzo, Paul Chagonja jana aliwasili hapa na kusema polisi watakabiliana na yeyote atakayejaribu kuanzisha vurugu.“Nasema vurugu sasa basi na ninaonya yeyote atakayejaribu kutuchokoza tutakabiliana naye kwa nguvu zote… wananchi waende kwa uhuru vituoni kupiga kura,” alisema.

Kwa upande wake, Naibu Kamishina wa Polisi anayeratibu usalama Igunga, Isaya Mngulu amesema polisi wamefungua vituo tisa kwa ajili ya kukabiliana na matukio ya vurugu yatakayojitokeza.

Alisema vituo hivyo vina vifaa vyote vya kisasa yakiwamo mabomu ya kutoa machozi na maji ya kuwasha na kwamba vikosi vimejizatiti kukabiliana na hali yoyote ya vurugu itakayojitokeza.

Alivitaja vituo hivyo kuwa vipo katika maeneo ya Simbo, Mwisi, Nkinga, Sungwisi, Ziba, Mwanshimba na Itumba na kwamba kila kituo kina polisi wa kutosha wenye uzoefu wa kukabiliana na kila aina ya vurugu.

Katika kuhakikisha kuwa uchaguzi huo unafanyika kwa amani na usalama, askari mgambo 325, Magereza wanane na polisi 94 watatumika katika kusimamia zoezi la upigaji kura katika vituo vyote 427.

Maandalizi yakamilika
Msimamizi wa Uchaguzi Igunga, Protas Magayane alisema jana kwamba vifaa vyote kwa ajili ya upigaji kura vipo tayari na vitaanza kusambazwa katika vituo vyote Jumamosi.

Magayane alisema orodha ya wapiga kura itabandikwa vituo kesho Alhamisi na kuwataka wale wote waliojiandikisha waende kuhakikisha majina yao na kufahamu vituo watakavyotumia kupiga kura.

Alisema wasimamizi wa vituo vya uchaguzi wapatao 427 waliapishwa jana na kwamba NEC itafanya kikao na viongozi wa vyama vyote vya siasa vinavyoshiriki katika uchaguzi huo ili kuwekana sawa.

CUF nayo yapata homa
CUF nacho kimetoa shutuma mbalimbali dhidi ya CCM ikiwamo ya kuingiza makontena ya sukari wilayani Igunga kwa lengo la kugawa kwa wananchi kama njia ya kurubuni wananchi wakipigie kura.

Tuhuma nyingine za CUF kwa CCM ni kuwa  kinatarajia kuingiza kundi la makomandoo waliomaliza mafunzo na semina katika Mkoa wa Shinyanga kwa ajili ya kuwatisha wapiga kura siku za mwisho za kampeni na uchaguzi.

Tuhuma hizo zilitolewa jana Mtatiro alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa.

Alisema tayari chama hicho kimepata taarifa za kuaminika kuwa kuna makontena yanayotarajia kusafirishwa kutoka Mara kwenda Igunga kwa ajili ya kugawanywa kwa wapiga kura. Bila kutaja kiasi alisema zinatarajiwa kuingia Septemba 29.

“Hii ni rushwa, haiwezekani kipindi hiki cha uchaguzi Serikali ya CCM kuleta kontena za sukari... tunataka Igunga ipate mbunge halali atakayechaguliwa na wananchi na sisi tumejipanga kuzuia jaribio hilo,” alisema Mtatiro.

Pia alidai kwamba chama hicho kimepanga kugawa chakula cha msaada nyumba kwa nyumba siku moja kabla ya kupiga kura na kwamba mpango huo umekamilika na magari yameandaliwa kufanya kazi hiyo Septemba 31 na Oktoba Mosi.

Akijibu tuhuma hizo Mratibu wa Kampeni wa CCM, Mwigulu Nchemba alikanusha na kusema wapinzani wao hao wana maralia ya uchaguzi.

Nchemba alisema kambi inayodaiwa ilifanyika siku nyingi na shughuli zake ziliisha... “Kambi tulishamaliza na sasa hakuna kinachoendelea, CCM hatuna mpango wa kuingiza vijana katika mji huu kutoka nje kwa ajili ya uchaguzi.”

Kuhusu chakula alisema Serikali imekuwa ikigawa chakula cha msaada katika maeneo mbalimbali yenye njaa na ilianza kufanya kazi hiyo kabla ya uchaguzi.

“Wanasema tunataka kugawa chakula Septemba 31 na Oktoba Mosi hapa Igunga? Siyo kweli kama tunafanya hivyo kwa ajili ya uchaguzi. Serikali inagawa chakula cha msaada katika maeneo yote ya njaa ikiwamo Igunga” alisema Nchemba.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP

Tuesday, July 5, 2011

TAHADHARI ,NAMATAPELI ,DEMOLINE LIQUID  DAWA ZA  VILIMO hapa dar 
kunamatapeli wa dawa za damoline liquid ,wakikuambia kuhusu madawa hayo ya damoline liquid matapeli hao wanjua mpaka majina wanafuatilia mpaka unavyo ishi jina na kadhalika epukana na hao watu pia wamejaribu hata mimi wakakuta mimi nina waelewa watu hao

Thursday, February 17, 2011

Dar Airport closed


Thursday, 17 February 2011 08:47 Authorities have temporarily closed the Julius Nyerere International Airport over safety concerns following powerful explosions at a nearby arms depot. No aircraft has landed or took off since 9pm Wednesday.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP

Hundreds stream back home

Thursday, 17 February 2011 09:04 Hundreds of residents of Gongo la Mboto, Ukonga, Airport, Kipawa, Pugu and surrounding areas who abandoned their houses following powerful explosions from an arms depot, have started to return to their homes. Many people were seen in bus stops, asking for more information about the safety of the area before they boarded buses heading to Gongo la Mboto.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP

Thursday February 17, 2011 Local News 20 dead, airport closed due to Dar es Salaam bomb explosion -- PM

By JIANG ALIPO in Dodoma, 17th February 2011 @ 04:52, Total Comments: 2, Hits: 800

At least twenty people are confirmed dead, while the Mwalimu Julius Kambarage Nyerere International Airport remains closed and about 4,000 displaced people are camping at the Uhuru Stadium following a massive bomb explosion at the Gongo la Mboto Military Camp in Dar es Salaam on Wednesday.

Reading a statement on the explosion which rocked the biggest city in the country, Prime Minister Mizengo Pinda, told the National Assembly here on Thursday morning that the explosions begun at the Tanzania People’s Defence Force (TPDF) camp storage warehouse number five on Wednesday evening.

“At 8:20pm the first explosion was heard from storage warehouse number five which stores bullets and other heavy ammunition. It didn’t take long before the explosion spread to 22 other warehouses at the camp,” said the PM.

The Prime Minister told the National Assembly that the explosions, which led to total destruction of 22 warehouses and partial destruction of one, continued to the early hours of Thursday morning.

“Early reports show that up to this morning (Thursday) at 5am several people were confirmed dead; 13 bodies were brought at the Amana Hospital, two at Temeke Hospital and other two at Muhimbili National Hospital.

“Unconfirmed reports also show that there are three deaths in Kitunda area. But we expect numbers to rise,” said the Prime Minister, adding that the hospitals received about 145 injured, who are also expected to increase.

Moreover, the National Assembly was told that the Mwalimu JK Nyerere airport is temporary closed due to unconfirmed reports that some bombs landed at the airport which is situated close to the camp.

“Due to that airplanes were not allowed to land since last night, and the airport is temporary closed until field engineers scan the area to make sure it is safe,” he said.

Moreover, Mr Pinda said that two soldiers' hostels were destroyed in the camp, but the soldiers staying inside managed to escape unharmed.

“Outside the camp, early assessment show that two nearby houses were completely destroyed, while one bomb landed in a classroom at a nearby secondary school, but nobody was harmed. Today we will continue to assess the damage," said Mr Pinda.

The Prime Minister further said that the army has advised people living near the camp to stay away from the area for their safety, meanwhile some 4,000 people are camping at the Uhuru Stadium. Moreover, people are also advised not to pick any unidentified metal, as it may be a bomb waiting to explode.

The government has given condolences to all people affected, promising that the army will investigate the issue.

Schools closed for fear of more explosions

Thursday, 17 February 2011 11:04
A number of primary and secondary schools located near the TPDF army camp where explosions occurred Wednesday night have been closed temporarily. Reports indicate that students and pupils have been ordered to go home for fear of further explosions. Affected schools include Abuu Juma secondary school in Kitunda suburb, Chanzige secondary school in Kisarawe and several others in Gongo la Mboto, Pugu and Ukonga.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
Last Updated on Thursday, 17 February 2011 12:44

150 children missing

Thursday, 17 February 2011 11:07
Red Cross officials have reported that at least 150 children have been reported missing. The Red Cross disaster Response manager, Kibar Tawakal said they have collected 150 children at the National Stadium where a temporary camp has been set to assist the victims.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP